WRRB YAWANOA WATENDAJI WA GHALA KUELEKEA MSIMU WA KOROSHO 2026/27
BODI ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) imeanza kuwapatia mafunzo watendaji wa ghala zaidi ya 100 kwa ajili ya msimu wa korosho wa 2026/27, huku ikiahidi kuimarisha usimamizi wa ubora wa zao hilo ili kukidhi viwango vya soko la ndani na kimataifa.
Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo ya siku tano kwa watendaji wa ghala mkoani Mtwara leo Septemba 14, 2026, Kaimu Mkurugenzi wa Uratibu Huduma wa WRRB, Mwita Thomas, amesema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo na kuongeza uelewa wa namna ya kusimamia ghala na kuhakikisha korosho zinazopokelewa na kuhifadhiwa zinakidhi viwango vya ubora kwa mujibu wa miongozo iliyopo.
“Mafunzo haya yatakuwa chachu kwa washiriki katika kuongeza tija na kuimarisha usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala katika zao la korosho,” amesema Bw. Thomas.
Amesema usimamizi madhubuti wa maghala ni muhimu katika kulinda ubora wa korosho na kuongeza ushindani wa zao hilo katika soko, hatua inayotarajiwa kuongeza manufaa kwa wadau wa mnyororo wa thamani.
Aidha, amewahakikishia wanunuzi watakaoshinda katika minada ya korosho kuwa WRRB itaendelea kusimamia ubora wa zao hilo kwa kuzingatia viwango vinavyotakiwa ili kuhakikisha wanapata bidhaa yenye ubora unaolingana na taarifa zilizotolewa wakati wa biashara.
Waziri Mkuu Asema Asilimia 20 ya Mapato ya Mazao Ielekezwe Kwenye Ujenzi wa Maghala Karibu na Wakulima
SIKU YA PILI YA MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA WRRB YAONESHA MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA BIASHARA YA MAZAO NA UCHUMI WA TAIFA
SIKU YA PILI YA MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA WRRB YAJADILI FURSA ZA BIASHARA ZA KIKANDA
SIKU YA PILI YA MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA WRRB YAJADILI FURSA ZA BIASHARA ZA KIKANDA
Miaka 20 ya Mfumo wa Stakabadhi za Ghala: Naibu Waziri Londo Ahamasisha Ushirikiano kwa Ukuaji wa Uchumi
WATUMISHI WA WRRB WAFANYA UTALII WA NDANI HIFADHI YA TAIFA YA MIKUMI
Bodi ya Stakabadhi za Ghala ni taasisi iliyochini ya wizara ya viwanda na biashara. Taasisi hii ilianzishwa chini ya Warehouse Receipts Act No. 10 ya mwaka 2005 na Act No 3 ya 2015 iliyorekebishwa 2016. Kazi ya taasisi ni kusimamia na kuhamasisha matumizi ya mfumo wa stakabadhi ghalani unaohakikisha...